Fadhila za Tawhid

أعرض المحتوى باللغة العربية anchor

translation Mwandishi :

<ul></ul><div class="ltr start"><div class="rtl start"><p class="ltr center" id="p1"><span dir="rtl">بسم الله الرحمن الرحيم</span></p><p class="ltr center" id="p2">Fadhila Za Tawhiyd.</p><p class="ltr center" id="p3">Imeandaliwa na alhidaaya.com</p><p class="ltr center" id="p4">Imepitiwa na Yunus Kanuni Ngenda.</p><p class="ltr left" id="p5">Anasema Allaah <span class="c2">(Subhaanahu wa Ta’alaa)</span>:</p><p class="rtl left" id="p6">فَاعْلَمْ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا اللَّـهُ</p><p class="ltr justify" id="p7">Basi elewa kwamba laa ilaaha illa-Allaah <span class="c2">(hapana mungu anayestahiki kuabudiwa kwa haki ila Allaah)</span><span class="c5">[Muhammad: 19]</span></p><p class="ltr justify" id="p8">Maana ya Tawhiyd kama alivyosema ‘Allaamah ‘Abdir-Rahmaan Naaswir As-Sa’dy katika <span class="c1">“Al-Qawlus-Sadiyd Fiy Maqaaswidit-Tawhiyd - Sharh Kitaab At-Tawhiyd”</span></p><p class="ltr justify" id="p9"><span class="c1">“Tambua kwamba maana ya Tawhiyd haina mipaka. Ni maarifa na kukiri kumpwekesha Ar-Rabb <span class="c2">(Mola)</span> kwa Swifa za ukamilifu, na kuthibitisha kwamba Anapwekeshwa katika Sifa Zake Adhimu na Tukufu, na kumpwekesha katika ‘ibaadah zote”</span>.</p><p class="ltr justify" id="p10">Kinyume cha Tawhiyd ni ‘Shirk’ ambayo ni kumshirikisha Allaah <span class="c2">(Subhaanahu wa Ta’alaa)</span> katika hayo yaliyotajwa yote yanayomuhusu Yeye Pekee.</p><p class="ltr justify" id="p11">‘Ulamaa wameigawanywa Tawhiyd katika sehemu tatu:</p><p class="ltr justify" id="p12">1 – Tawhiyd Ar-Rubuwbiyyah</p><p class="ltr justify" id="p13">Nayo ni kumpwekesha Allaah katika Uumbaji, Uendeshaji wa mambo yote katika Ulimwengu, Utoaji rizki, Uletaji uhai na Ufishaji, kwa kuamini kwamba Yeye Ndiye Aliyeumba kila kitu, Anayeruzuku na kuendesha mambo yote ni Allaah <span class="c2">(Subhaanahu wa Ta’alaa)</span>. Hana mshirika,<span class="c6"> na kuamini kwamba Ufalme wote ni wake:</span></p><p class="ltr justify" id="p14">Allaah <span class="c2">(Subhaanahu wa Ta’alaa)</span> Anasema:</p><p class="rtl justify" id="p15">قُلْ مَن رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ قُلِ اللَّـهُ ۚ</p><p class="ltr justify" id="p16">Sema: "Ni nani Mola wa mbingu na ardhi?" Sema: "Ni Allaah" <span class="c5">[Ar-<span class="c6">Ra’d:</span>16]</span></p><p class="ltr justify" id="p17">Na Anasema:</p><p class="rtl justify" id="p18">قُلْ مَن يَرْزُقُكُم مِّنَ السَّمَاءِ وَالْأَرْضِ أَمَّن يَمْلِكُ السَّمْعَ وَالْأَبْصَارَ وَمَن يُخْرِجُ الْحَيَّ مِنَ الْمَيِّتِ وَيُخْرِجُ الْمَيِّتَ مِنَ الْحَيِّ وَمَن يُدَبِّرُ الْأَمْرَ ۚ فَسَيَقُولُونَ اللَّـهُ ۚ فَقُلْ أَفَلَا تَتَّقُونَ</p><p class="ltr justify" id="p19">Sema: <span class="c1">“Nani anayekuruzukuni kutoka mbinguni na ardhini. Au nani anayemiliki kusikia na kuona; na nani anayemtoa <span class="c2">(aliye)</span> hai kutoka mfu, na anayemtoa mfu kutoka <span class="c2">(aliye)</span> uhai; na nani anayedabiri mambo <span class="c2">(yote)</span>? Watasema: “Ni Allaah”</span>; basi sema: <span class="c1">“Je basi hamuwi na taqwa?”</span> <span class="c2">(Hamumkhofu Allaah?)</span> <span class="c5">[Yunus: 31]</span></p><p class="ltr justify" id="p20">2-Tawhiyd Al-Uluwhiyyah</p><p class="ltr justify" id="p21">Maana yake ni kumwepekesha Allaah katika 'ibaadah na kuzielekeza ‘ibaadah zote kwa Allaah <span class="c2">(Subhaanahu wa Ta’alaa)</span>.</p><p class="ltr justify" id="p22">Allaah <span class="c2">(Subhaanahu wa Ta’alaa)</span> Anasema:</p><p class="rtl justify" id="p23">قُلْ إِنَّ صَلَاتِي وَنُسُكِي وَمَحْيَايَ وَمَمَاتِي لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿١٦٢﴾ لَا شَرِيكَ لَهُ ۖ وَبِذَٰلِكَ أُمِرْتُ وَأَنَا أَوَّلُ الْمُسْلِمِينَ ﴿١٦٣﴾</p><p class="ltr justify" id="p24">Sema: <span class="c1">“Hakika Swalaah yangu, na nusukiy <span class="c2">(kuchinja kafaara na ‘ibaadah zangu)</span> na uhai wangu na kufa kwangu ni kwa ajili ya Allaah <span class="c2">(Pekee)</span> Mola wa walimwengu.”</span> Hana mshirika, na kwa hayo ndio nimeamrishwa, nami ni Muislamu wa kwanza <span class="c2">(waliojisilimisha kwa Allaah)</span>. <span class="c5">[Al-<span class="c6">An’aam:</span> 162-163]</span></p><p class="ltr justify" id="p25">3-Tawhiyd Asmaa wasw-Swifaat</p><p class="ltr justify" id="p26">Kumpwekesha Allaah <span class="c2">(Subhaanahu wa Ta’alaa)</span> kwa Sifa Zake Tukufu, na Majina Yake mazuri, bila kuzigeuza Sifa hizo maana zake, au kuzipinga, au kuzifananisha na viumbe au kuzipa unamna. Yeye Amejipa Majina mazuri mazuri na Sifa nzuri nzuri na Akawataka waja Wake wamuombe na kumtukuza kwa Majina na Sifa hizo.</p><p class="ltr justify" id="p27">Allaah <span class="c2">(Subhaanahu wa Ta’alaa)</span> Anasema:</p><p class="rtl justify" id="p28">وَلِلَّـهِ الْأَسْمَاءُ الْحُسْنَىٰ فَادْعُوهُ بِهَا ۖ وَذَرُوا الَّذِينَ يُلْحِدُونَ فِي أَسْمَائِهِ ۚ سَيُجْزَوْنَ مَا كَانُوا يَعْمَلُونَ ﴿١٨٠﴾</p><p class="ltr justify" id="p29">Na Allaah Ana Majina Mazuri kabisa, basi muombeni kwayo. Na waacheni wale wanaopotoa <span class="c2">(kwa kuharibu utukufu, kukanusha, kugeuza maana, kushabihisha)</span> katika Majina Yake, watalipwa yale waliyokuwa wakiyatenda. <span class="c5">[Al-<span class="c6">A’raaf:</span> 180]</span></p><p class="ltr justify" id="p30">Qur-aan nzima imedhihirisha Tawhiyd ya Allaah <span class="c2">(Subhaanahu wa Ta’ala)</span>; mfano Suwratul-Faatihah ambayo tunaisoma kila siku mara kumi na saba katika Swalaah zetu za fardhi na pia katika Swalaah zote nyinginezo, imejumuisha aina tatu zote za Tawhiyd.</p><p class="rtl justify" id="p31">بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ ﴿١﴾ الْحَمْدُ لِلَّـهِ رَبِّ الْعَالَمِينَ ﴿٢﴾ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ ﴿٣﴾ مَالِكِ يَوْمِ الدِّينِ ﴿٤﴾ إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ ﴿٥﴾</p><p class="ltr justify" id="p32">Kwa Jina la Allaah Ar-Rahmaanir-Rahiym <span class="c2">(Mwingi wa Rahmah - Mwenye kurehemu)</span>. AlhamduliLLaahi <span class="c2">(Sifa njema zote ni za Allaah)</span> Mola wa walimwengu. Ar-Rahmaanir-Rahiym <span class="c2">(Mwingi wa Rahmah-Mwenye kurehemu)</span>. Maalik <span class="c2">(Mfalme)</span> wa siku ya malipo. Wewe Pekee tunakuabudu na Wewe Pekee tunakuomba msaada <span class="c5">[Al-<span class="c6">Faatihah:</span> 1-5]</span></p><p class="ltr justify" id="p33">Na pia kauli ya Allaah <span class="c2">(Subhaanahu wa Ta’ala)</span>:</p><p class="rtl justify" id="p34">رَّبُّ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضِ وَمَا بَيْنَهُمَا فَاعْبُدْهُ وَاصْطَبِرْ لِعِبَادَتِهِ ۚ هَلْ تَعْلَمُ لَهُ سَمِيًّا ﴿٦٥﴾</p><p class="ltr justify" id="p35">Mola wa mbingu na ardhi na vilivyo baina yake; basi mwabudu Yeye tu na dumisha subira katika ‘ibaadah Yake. Je, unamjua <span class="c2">(mwengine)</span> mwenye Jina Lake? <span class="c2">(Bila shaka hakuna aliyefanana Naye kwa lolote, vyovyote, na wala hana mshirika!)</span>. <span class="c5">[Maryam: 65]</span></p></div></div>

1

Fadhila za Tawhid

3.6 MB DOCX
2

Fadhila za Tawhid

381.6 KB PDF

Jamii ya vilivyomo