<ul></ul><div class="ltr start"><div class="rtl start"><p class="rtl center" id="p1">بسم الله الرحمن الرحيم</p><p class="ltr center" id="p2">NYAKATI TATU MUHIMU ZA IBADA ZISIKUPITE KATIKA RAMADHANI</p><p class="ltr left" id="p3">Imeandaliwa na Alhidaya.com</p><p class="ltr left" id="p4">Imepitiwa na Abubakari shabani Rukonkwa</p><p class="ltr justify" id="p5">Nyakati tatu hizi ni muhimu sana za kufanya ibada kutokana na fadhila zake kuu. Mwenye kupenda kuchuma thawabu nyingi asizikose khaswa katika mwezi huu Mtukufu Wa Ramadhaan ambao ni mwezi wenye malipo maradufu</p><p class="ltr justify" id="p6">1-<span class="c6">Wakati wa mwanzo:</span> Baina ya Alfajiri na jua kuchomoza:</p><p class="ltr justify" id="p7">Usimulizi uliothibiti kutoka katika Swahiyh Muslim <span class="c2">(564/1)</span> kwamba Mtume <span class="c2">(Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)</span> na Maswahaba walikuwa wakibakia macho wakati huo hadi jua kuchomoza kwani ni wakati mja anapogaiwa rizki yake, na ni wakati wenye kheri nyingi, unampa siha nzuri ya mwili binaadamu, na kwa ujumla ni wakati wenye baraka nyingi za kila aina kwani Mtume <span class="c2">(Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)</span> aliomba:</p><p class="rtl justify" id="p8"><span class="c2">((اللهم بارك لأمتي في بكورها)</span>) الترمذي, أحمد, أبي داود, ابن ماجه</p><p class="ltr justify" id="p9"><span class="c2">((Ee Allaah, wabarikie Ummah wangu nyakati za asubuhi mapema)</span>) <span class="c5">[At-Tirmidhiy, Ahmad, Abu Daawuud, Ibn Maajah na imethibitishwa kuwa ni Hadiyth Swahiyh na Shaykh Al-Albaaniy]</span></p><p class="ltr justify" id="p10">Usimulizi huu umetoka kwa Maswahaba kadhaa ambao wameelezea kwamba: "Mtume <span class="c2">(Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)</span> alipotaka kupeleka kikosi au jeshi aliwapeleka mwanzo wa asubuhi".</p><p class="ltr justify" id="p11">Vile vile wamesimulia kwamba:"Swakhar alikuwa mtu tajiri ambaye alikuwa akipelekea biashara zake mwanzo wa asubuhi na matokeo yake ilikuwa ni kufuzu katika biashara na kupata faida kubwa sana".</p><p class="ltr justify" id="p12">Wamesimulia Salafus-<span class="c6">Swaalih kwamba Ibn 'Abbaas naye alimkataza mtu kulala nyakati hizo alipomwambia:</span></p><p class="rtl justify" id="p13">"قُم، أتنام في الساعة التي تقسَّم فيه الأرزاق؟"</p><p class="ltr justify" id="p14">"Inuka! Je, unalala katika saa ambayo rizki inagaiwa?"</p><p class="ltr justify" id="p15">Ikiwa wakati huo ni kama hivyo ilivyoelezwa juu, basi vipi Muislamu aache wakati huu umpite hasa katika mwezi huu mtukufu wa Ramdhaan?</p><p class="ltr justify" id="p16">Ibnul-Qayyim <span class="c2">(Rahimahu-Allaah)</span> katika kitabu chake 'Zaad Al-<span class="c6">Ma'aad' amesema:</span> "Usingizi wa asubuhi unanyima rizki kwani huo ni wakati ambao Muumba anaombwa rizki na wakati wa kugaiwa rizki. Hivyo usingizi unanyima rizki isipokuwa kwa dharura. Usingizi wakati huo pia ni madhara kwa mwili…"</p><p class="ltr justify" id="p17">Faida nyingine kubwa ya kubakia macho ukimdhukuru Allaah wakati huu:</p><p class="ltr justify" id="p18">Kwa muda wa saaa moja na nusu takriban utakuwa umepata thawabu za Hajj na ‘Umrah zikiwa kamilifu:</p><p class="rtl justify" id="p19">عن أنس عن النبي صلى الله عليه وسلم ، أنه قال <span class="c2">(( من صلى الفجر في جماعة ثم قعد يذكر الله حتى تطلع الشمس ثم صلى ركعتين كانت له كأجر حجة وعمرة تامة تامة تامة)</span> ) أخرج الترمذي صححه الألباني .</p><p class="ltr justify" id="p20">Imetoka kwa Anas kwamba Mtume <span class="c2">(Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)</span> amesema: <span class="c2">((Atakayeswali Alfajiri katika Jamaa'ah kisha akakaa anamdhukuru Allaah mpaka likachomoza jua kisha akaswali Raka'ah mbili, atapata ujira kama ujira wa kwenda Hajj na 'Umrah ulio kamili kamili kamili)</span>) <span class="c5">[Imetolewa na At-Tirmidhiy na kaisahihisha Al-Albaaniy]</span></p><p class="ltr justify" id="p21">Pindi ukifanya hivyo kwa mwezi mzima utakuwa umechuma thawabu za Hajj na ‘Umrah za muda wa mwezi mzima. Hizo ni fadhila za siku za kawaida, seuze ukifanya mwezi mtukufu huu wa Ramadhaan? Jitahidi ndugu Muislamu kadiri uwezavyo kuchuma hizi thawabu kubwa ambazo zingelikukalifu mali, tabu za safari na mashaka ya kufika Makkah kutekeleza ibada hizo. Lakini kwa Rehma ya Allaah Amejaalia thawabu hizo ziweze kuchumwa tukiwa majumbani mwetu tena kwa wepesi kabisa. Wanaume inawapasa waswali msikitini kuzipata thawabu hizo kwa kuwa Hadiyth imetaja atakayeswali jamaa’ah. Ama wanawake, wanazipata fadhila hizo hata wakiswali majumbani mwao. Hata hivyo, juu ya kuweko fadhila kama hiyo, tusisahau kuwa haivunji wala haifuti fardh ya kwenda Hajj kwa mwenye uwezo, asije mtu akadhani kufanya hayo kutakuwa kumetengua wajibu wake wa kuhiji au kufanya ‘Umrah.</p><p class="ltr justify" id="p22">2-<span class="c6"> Wakati wa pili:</span> Kabla ya Jua kuzama <span class="c2">(Magharibi)</span>:</p><p class="ltr justify" id="p23">Huu ni wakati ambao bado Muislamu yuko katika Swawm na du'aa yake anayoiomba hairudi:</p><p class="rtl justify" id="p24">قال صلى الله عليه وسلم: <span class="c2">((ثَلاثةٌ لا تُرَدُّ دعوتُهم: الصَّائم حتَّى يُفْطِر، والإمام العادِل، ودعْوة المظْلوم)</span>) وروى الترمذي بسند حسن</p><p class="ltr justify" id="p25">Mtume <span class="c2">(Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)</span> amesema: <span class="c2">((<span class="c5">[Watu]</span> watatu du'aa zao hazirudi; mwenye kufunga Swawm hadi afuturu. Kiongozi muadilifu na aliyedhulumiwa)</span>) <span class="c5">[At-Tirmidhiy kwa isnaad nzuri]</span></p><p class="ltr justify" id="p26">Ni fursa kwa Muislamu atumie wakati huo kuomba du'aa wakati huu hasa kwa vile ni wakati ambao Allaah <span class="c2">(Subhaanahu wa Ta'ala)</span> Amehimiza Atukuzwe kama Anavyosema:</p><p class="rtl justify" id="p27">وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ قَبْلَ طُلُوعِ الشَّمْسِ وَقَبْلَ الْغُرُوبِ</p><p class="ltr justify" id="p28">... na msabbih kwa kumsifu Mola wako kabla ya kuchomoza jua na kabla ya kuchwa <span class="c5">[Qaaf: 39]</span></p><p class="rtl justify" id="p29">وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ قَبْلَ طُلُوعِ الشَّمْسِ وَقَبْلَ غُرُوبِهَا وَمِنْ آنَاء اللَّيْلِ فَسَبِّحْ وَأَطْرَافَ النَّهَارِ لَعَلَّكَ تَرْضَى</p><p class="ltr justify" id="p30">…Na msabbih Mola wako kwa kumsifu kabla ya kuchomoza jua, na kabla halijachwa, na nyakati za usiku pia umsabbih na ncha za mchana ili upate ya kukuridhisha <span class="c5">[Twaahaa: 130]</span>.</p><p class="rtl justify" id="p31">وَاسْتَغْفِرْ لِذَنبِكَ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ بِالْعَشِيِّ وَالْإِبْكَار</p><p class="ltr justify" id="p32">Na omba maghfirah kwa dhambi zako, na umsabbih Mola wako kwa kumsifu jioni na asubuhi)) <span class="c5">[Ghaafir: 55]</span></p><p class="ltr justify" id="p33">3-<span class="c6"> Wakati wa tatu:</span> Suhuur - Kabla ya Alfajiri</p><p class="ltr justify" id="p34">Allaah <span class="c2">(Subhaanahu wa Ta'ala)</span> Amewaaahidi wenye taqwa Pepo kwa sababu miongoni mwa sifa zao ni kuomba maghfira kabla ya Alfajiri:</p><p class="rtl justify" id="p35">إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُون. آخِذِينَ مَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَلِكَ مُحْسِنِينَ. كَانُوا قَلِيلًا مِّنَ اللَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ. وَبِالْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُون.</p><p class="ltr justify" id="p36">Hakika wenye taqwa watakuwa katika Jannaat na chemchem. Wanapokea Aliyowapa Mola wao. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema. Walikuwa wakilala kidogo tu usiku. Na kabla ya Alfajiri wakiomba maghfira. <span class="c5">[Adh-<span class="c6">Dhaariyaat:</span> 15-18]</span></p><p class="ltr justify" id="p37">Kisha wamesifiwa tena kwa sifa kama hiyo pamoja na nyinginezo:</p><p class="rtl justify" id="p38">الصَّابِرِينَ وَالصَّادِقِينَ وَالْقَانِتِينَ وَالْمُنفِقِينَ وَالْمُسْتَغْفِرِينَ بِالأَسْحَارِ</p><p class="ltr justify" id="p39">Wanaosubiri, wanaosema kweli, na watiifu, na wanaotoa sadaka, na wanaoomba maghafira kabla ya Alfajiri.<span class="c5">[Al-<span class="c6">'Imraan:</span> 17]</span></p><p class="ltr justify" id="p40">Muislamu asiache wakati huo umpite kwani ni wakati muhimu na wenye fadhila na faida kubwa kwa vile Allaah <span class="c2">(Subhaanahu wa Ta'ala)</span> Huteremka wakati huo kutoka mbingu ya saba na kuweko mbingu ya ardhi kututakabalia maombi ya anayemuomba:</p><p class="rtl justify" id="p41">عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: <span class="c2">((يَنْزِلُ رَبُّنَا تَبَارَكَ وَتَعَالَى كُلَّ لَيْلَةٍ إِلَى السَّمَاءِ الدُّنْيَا حِينَ يَبْقَى ثُلُثُ اللَّيْلِ الْآخِرُ يَقُولُ: مَنْ يَدْعُونِي فَأَسْتَجِيبَ لَهُ مَنْ يَسْأَلُنِي فَأُعْطِيَهُ مَنْ يَسْتَغْفِرُنِي فَأَغْفِرَ لَهُ)</span>) البخاري و مسلم</p><p class="ltr justify" id="p42">Imetoka kwa Abu Hurayrah <span class="c2">(Radhiya Allaahu 'anhu)</span> kwamba Mtume <span class="c2">(Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam)</span> amesema: <span class="c2">(Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)</span> Huteremka <span class="c2">(kwa namna inavyolingana na utukufu Wake)</span> kila siku katika mbingu ya dunia <span class="c2">(mbingu ya kwanza)</span> inapobakia thuluthi ya mwisho ya usiku na Husema: Nani ananiomba Nimtakabalie? Nani ana shida Nimtekelezee? Nani ananiomba maghfirah Nimghufurie?)) <span class="c5">[Al-Bukhaariy na Muslim]</span></p><p class="ltr justify" id="p43">Nani miongoni mwetu asiyemhitaji Mola wake kumtakabalia haja zake au kumuondeshea shida zake? Nani asiyekuwa na madhambi asiyemhitaji Mola wake kumghufuria? Hivyo usiache wakati huu ukakupita hasa kwa vile ni mwezi wa Ramadhaan ambao kila jambo ulifanyalo lina fadhila na thawabu marudufu.</p><p class="ltr justify" id="p44">Tunamuomba Allaah <span class="c2">(Subhaanahu wa Ta'ala)</span> Atuwezeshe kudiriki nyakati hizo tatu na nyingine, tuwe katika ibada katika mwezi huu wa Ramadhaan na miezi yote mingineyo na Atujaalie kheri na Baraka nyingi, Atutakabalie haja zetu, Atuondoshee shida zetu na Atughufurie madhambi yetu yote. Aamiyn.</p></div></div>
1
NYAKATI TATU MUHIMU ZA IBADA ZISIKUPITE KATIKA RAMADHANI
2
NYAKATI TATU MUHIMU ZA IBADA ZISIKUPITE KATIKA RAMADHANI