×
Hiki ni kitabu kilichotayarishwa kwa lengo la kuwapatia wasomaji, suluhisho la matatizo wanayoyapata watu wengi wanapotaka kufahamu ni ipi Dini ya Haki.

 RISALA FUPI YA KUMUWEZESHA MTU KUPAMBANUA NI IPI DINI YA HAKI

 

 NI IPI DINI YA HAKI

 UTANGULIZI

Kama inavyojulikana, katika dunia kunazo Dini nyingi sana lakini katika Dini hizo zote, kunazo tatu (mashuhuri) ambazo zinao uhusiano.

Dini zenyewe ni UYAHUDI, UKRISTO na UISILAMU.

 SEHEMU YA KWANZA

UHUSIANO WAO NI UPI?

Kwanza: Mungu wao, aliyetajwa katika vitabu vyao, ni MUNGU WA MBINGUNI.

(hivi kwamba, hata akisikika yeyote katika wafuasi wa Dini hizi akisema “Mungu wangu” au “Mungu wetu ni fulani wa fulani,” itabaki katika vitabu vyao kwamba, Mungu wa mbinguni ndiye pekee Mungu wa kweli.)

(38)
(Wayahudi, wafarisayo)
(Yesu)

.

 SEHEMU YA PILI

Uhusiano wa pili: Upo katika Mitume wa Mungu ( huyu wa Mbinguni ).

Kwa mfano, utaona katika mafundisho ya Dini hizi, Adam na mkewe Hawa wametajwa kwamba ndio watu wa kwanza.

Mtume Nuhu, kwa mfano mwengine, utaona ametajwa kote kote kwamba, alitengeneza Safina kwa amri ya Mungu na Watu wa enzi yake wakaangamizwa kwa mvua kali na mafuriko, kwa sababu ya kumuasi Mungu, na kutoamini maneno ya Nuhu.

Mitume wengine kama vile Nabii Ibrahim pia wametajwa, na Nabii Lut ambaye watu wa enzi yake waliangamizwa kwa sababu ya kumuasi Mungu, kwa kuwa walikuwa wakizini baina ya wanaume kwa wanaume wenzao, na walikataa pia kumtii Mtume wao Lut.

Mitume kama vile Yakubu (anayeitwa pia Israeli) ametajwa na wanawe akiwemo Yusuf (Joseph) na Benyamin (Benjamin). Kisa cha Yusuf kimetajwa tangu alipouzwa kama Mtumwa nchini Misri (kutokana na wivu wa ndugu zake) hadi akafikia kuwa kiongozi katika viongozi wa nchi hiyo.

Mtume Musa (Moses) na Daudi (David) na vile vile Suleiman (Solomon) wametajwa katika mafundisho ya Dini zote hizi, na Mitume wengineo.

JE TOFAUTI ZAO ZIPO WAPI?

 SEHEMU TA TATU

Je! walikuwa na sababu gani ya kuabudu sanamu?

Sanamu kama tunavyomjua anayo macho lakini je! anaona chochote kwa hayo macho? La! Na pia anayo masikio, je! anasikia chochote kwa hayo masikio? La! Na pia anao mdomo, je! anatamka chochote? La!

Sanamu akianguka kwa mfano, je! anaweza kujisaidia kwa kurudi alipokuwa? La!

Kwa hivyo, ikiwa tunajua kwamba sanamu hawezi hata kujisaidia mwenyewe, je! wanaomuabudu wakitaka awasadie huwa wanataraji sanamu ataweza kuwasaidia vipi?

 SEHEMU YA NNE

 Nehemia 9:16-17

 SEHEMU YA TANO

Basi (kizazi cha) Wayahudi hawa hawa walifanya na makosa mengine ya kuwa wanawauwa Manabii (waliotumwa na Mungu), mmoja baada ya mwengine, hadi mwisho wakafanya na kosa kubwa sana, kosa la kumkataa Mtume wa Mungu, Yesu kristo (Nabii Isa Mwana wa Mariam), na hali ya kuwa alikuwa ametumwa kwao. Na wao pia ndio waliopanga kumuuwa. (Ikiwa walifaulu au hawakufaulu kumuuwa, hayo tutayaona baadaye.)

Makosa ya Wayahudi hadi hapa tunaona kwamba, kwanza ni kuvunja Amri ya kwanza ya Mungu, kitendo kinachompelekea aliye kitenda kupata Laana kubwa, Laana ya Mungu, kama ilivyoandikwa katika Biblia,

Makosa ya pili ni kuwauwa Manabii waliotumwa na Mungu, kama kwamba Wayahudi hawa wanawaambia, “Maneno mliyokuja nayo, mkisema ni kutoka kwa Mungu, sisi tutawauwa kwa sababu maneno yenu (tunavyoyaelewa sisi) ni uwongo.”

Watu waliopata Laana ya Mungu, hujulikana kwa maneno yao au kwa vitendo vyao.

 SEHEMU YA SITA

Walipokataa Wayahudi kuipokea Injili ya Yesu, waliichukua Waroma kiasi walichoweza kuipata, kwa sababu wao ndio waliokuwa wakiwatawala Wayahudi enzi hizo.

Waroma kabla ya hapo walikuwa Makafiri (yaani watu wanoabudu sanamu na pia miungu wengi, hawafuati Mila ya Nabii Ibrahim, na kwa hivyo hawatahiri.) na wao ndio walioanzisha Dini ya ROMAN CATHOLIC.

Roman maana yake ni watu wa nchi ya Italia, yaani Wataliano. Na Catholic maana yake UNIVERSAL au INTERNATIONAL (UROMA WA KIMATAIFA).

Swali: je! Waroma waliendelea na kuhubiri Dini aliyokuwa akihubiri Yesu?

Au walichanganya mila yao na Dini hiyo mpya?

Je! Roman Catholic inamaanisha sote tuwe Wataliano?

Kama ni hivyo je! Ni ki-lugha au ki-tabia au ki-Ibada?

 (Yesu akasema) Msidhani ya kuwa nilikuja kuitangua Torati au manabii; La! Sikuja kuitangua bali kuitimiliza 18. Kwa maana, amin nawaambia, Mpaka Mbingu na Nchi zitakapoondoka, yodi moja au nukta moja ya Torati, haitaondoka hadi yote yatimie.

 SEHEMU YA SABA

Wakristo nao walifanya kama walivyofanya Wayahudi, kwa kumkataa Mtume wa mwisho Muhammad, Swalla Allahu alaihi wa sallam, alipotumwa, na hali kuja kwake kumetabiriwa katika TAURATI ya Wayahudi na INJILI.

 Kumbukumbu la Torati 18:17-19

Bwana akaniambia wametenda vyema kusema walivyosema 18 Mimi Nitawatolea Nabii miongoni mwa ndugu zao mfano wako wewe (Musa) Nami nitatia maneno yangu kinywani mwake, naye atawaambia yote nitakayowaamuru 19 hata itakuwa mtu asiyesikia maneno ya yangu atakayosema yule (Nabii) kwa jina langu, nitalitaka kwake.

Jiwe walilokataa waashi (mafundi) hilo ndilo limekuwa jiwe kuu la pembeni; Neno hili limetoka kwa Bwana, nalo ni ajabu machoni petu? 43 Kwa sababu hiyo nawaambia, Ufalme wa Mungu utaondolewa kwenu (Wayahudi) nao (huo ufalme) watapewa taifa lingine lenye kuzaa matunda yake

Sababu walizotoa viongozi wa kikristo za kumkataa Mtume Muhammad, Swalla Allahu alaihi wa sallam, zinafanana na zile walizotoa Wayahudi za kumkataa Yesu kristo. Na kama walizotoa viongozi wa Umma (yaani Generation) zote zilizo wapinga Mitume wao. (Yaani kumtangaza Mtume wa Mungu kuwa Muwongo, kumkadhibisha.)

Angalia Yohana 7:12

Utaona kwamba Wayahudi hawakuona kule kusema Yesu (Nabii Isa) ni muwongo, kuwa ni jambo kubwa au kuwa ni la ukafiri. Pamoja na ushahidi wote aliouleta na hasa kitabu cha Injili.

Wakristo nao walisema imeandikwa katika kitabu chao kwamba kutakuja mitume wa uwongo na wakawa wanasema Muhammad, Swalla Allahu alaihi wa sallam, ni mmoja wao.

 SEHEMU YA NANE

Sasa nasi hebu tuone, vipi tunaweza kumtambua Mtume wa kweli na wa uwongo katika hali kama hii?

Jawabu: hebu tazama mfano kama huu ufuatao;

Je! Akija leo mtu kwako na kusema kuwa yeye ni Polisi na kwamba unatakiwa uandamane naye hadi kituoni, wewe utafanya nini?

Utamwambia atoe kitambulisho cha kudhihirisha kuwa yeye ni Polisi au sivyo?

Kitambulisho cha Muhammad, Swalla Allahu alaihi wa sallam, ni QUR’AN.

Ambayo kama ingelitoka kwa asiyekuwa ALLAH (jina ambalo maana yake kwa lugha za mashariki ya kati, ni MOLA WA ULIMWENGU) ingepatikana ndani yake makosa mengi.

Na kwa sababu Muhammad, Swalla Allahu alaihi wa sallam, hajawahi kwenda shule na alikuwa hajui kusoma wala kuandika, vipi anaweza yeye kutunga kitabu, na hali ya kuwa utunzi wa vitabu ni kazi ya wasomi?

 SEHEMU YA TISA

Kitabu cha Qur’an kinatumika kumuongoza mtu hadi akafaulu kuishi maisha mema Duniani na Akhera (maisha ya baadaye). Kama kinavyotumika kuongoza Familia na hata kabila (Tribe).

Kisha kinatumika pia kuongoza nchi nzima, kwa kuwa kinatumika kama vile katiba.

Na pia kinao uwezo wa kuongoza Dunia yote, ki- jamii, ki- siasa, ki-uchumi, ki-utamaduni, ki-masomo, ki-mahakama, ki-ulinzi, na ni uongozi kwa kila aina ya mahitaji ya mwanadamu.

Kitabu hiki ni kidogo sana kwa umbo lake, lakini (amini au usiamini) ndicho kinachotumiwa (kama vile katiba) na baadhi ya nchi ambazo zimepiga hatua kubwa katika maendeleo ya kijamii, ki-uchumi, ki-elimu na ki-siasa duniani.

Je! Wewe mwenyewe umeona katiba ya kuongoza nchi inavyohitaji watu wengi (Ma-Profesa) ili kutayarisha, na kila baada ya miaka fulani, inasemekana hiyo katiba inayo makosa, inahitaji katiba mpya. Na hali walioitengeneza wote ni wataalamu waliomaliza muda mwingi kusoma.

(wakusaidieni)
( kuwa hakuteremshiwa na Mwenyezi Mungu )
(mtu)

  

 SEHEMU YA KUMI

Je! Si muujiza mtu anayelisha kondoo jangwani, asiyejua kusoma na kuandika, awe na uwezo wa kutunga katiba ya ulimwengu mzima?

katiba ambayo kwa miaka - sasa zaidi ya 1,400 - haijawahi kupatikana na makosa, wala kubadilishwa, wala kupunguka uwezo wake na hali yakuwa ni katiba ambayo mlinzi wake (kutokana na uadui wa binadamu) anakuwa ni ALLAH, hadi siku ya kiama?

Je! Kuna kitabu cha mtaalamu yeyote kimeshawahi kubadilisha fikra za watu ulimwenguni kama kilivyofanya kitabu cha Qur’an?

Biblia, pamoja na hali ya kuwa imeathiri watu wengi Duniani, lakini Je! inazo vitabu vya waandishi wangapi?

Kwa hivyo Qur’an ndio muujiza mkubwa wa Mtume Muhammad, Swalla Allahu alaihi wa sallam. Na ni muujiza mkubwa kuliko miujiza ya Mitume wote waliotangulia kwa sababu, ni muujiza wa kudumu hadi mwisho wa Dunia.

 SEHEMU YA KUMI NA MOJA

Kutokana na walivyofunza Mitume wa Mungu tangu wa mwanzo, yaani kuwapo Mungu mmoja, Mola wa ulimwengu wote, inaeleweka kutokana na mafunzo yao kwamba, Dini ya Adam, ndio pia Dini ya Nuhu, na ndio pia Dini ya Ibrahim na ndio Dini ya Mitume wote, (Amani ya ALLAH iwe juu yao).

Kwa hivyo Dini ya Muhammad, ndiyo pia Dini ya Adam na Hawa na ndiyo pia Dini ya Mitume wote. Kwa sababu hawezi mtu kuwa Muislamu hadi atakapokubali moyoni na kutamka kwa ulimi wake ukweli wa kuwapo Mungu mmoja, na kuamini Mitume wote.

Maana ya Islam ni pale Mtu anapoamua kuamini na kutii Amri zote za Mola wa Ulimwengu, kwa kupenda kwake (mwenyewe) bila kulazimishwa. Kwa hivyo mafunzo ya Muhammad hayapingani na mafunzo ya Mtume yeyote wa Allah, hata mmoja.

Kilichowapelekea viongozi wa Kikristo kumpinga Mtume Muhammad, Swalla Allahu alaihi wa sallam, ndicho hicho hicho kilichowapelekea viongozi wa kiyahudi kumpinga Yesu kristo ( Nabii Isa).

Kila Nabii wa Mungu alipata wapinzani kutoka kwa viongozi wa Watu wa enzi yao. Mahubiri yao yakawa yanakanushwa, na kufanyiwa kejeli, na matusi wametukanwa na baadhi yao wamepigwa na hata kuuawa.

 SEHEMU YA KUMI NA MBILI

Haya huwa yanatokana na Laana ya Mungu, wanayoipata viongozi hawa kwa sababu ya kuvunja amri ya Mungu ya kwanza na kutowaamini Mitume.

Kisha wakawa wanayapindua maneno ya Mungu, yakawa sio vile yalivyokuwa wakati wa Mitume. Kwa kuyaongeza, kuyageuza na kupachika maneno wayapendayo wao kisha wakasema, “Haya ndiyo maneno ya Mungu.”

Ikiwa kunapatikana ubishi kuhusu jambo hili, kwa kuwapo anayedai kwamba Biblia yote ni maneno ya Mungu na imetakasika, inafaa atazame mfano ulio wazi baina ya Biblia wanayoitumia Wakatoliki na ile ya Waprotestanti.

Kila mmoja wao hudai kwamba Biblia anayoitumia ndiyo takatifu.

Mkatoliki humlaumu Mprotestanti kwa kusababisha kupunguzwa maneno anayodai kuwa ni ya Mungu katika Biblia. Naye Mprotestanti hujitetea kwa kudai kwamba Biblia ya Mkatoliki inazo vitabu vingi ambavyo sio naneno ya Mungu.

Kwa hivyo ikiwa Biblia zinatofautiana hivyo, zitakuwa vipi zote takatifu?

Je! Ni nani huwa anayaongeza maneno ya Mungu, na ni nani huwa anayapunguza?

Haya mambo ya kujitafutia laana ya Mungu huwa yanawapelekea kusema na kutenda vitendo vilivyokosa muelekeo.

Kwa mfano, utamwelewa vipi Mtu ambaye anakusimulia kisa cha Mtu ambaye (msimuliaji asema) alikuwa ni mrefu kisha aseme pia alikuwa ni mfupi? Au Mtu mweupe lakini kwa hakika ni mweusi?

Muhubiri wa Kikristo huanza mahubiri yake kwa kusema kuwa “Mungu ni Mmoja.”

Kisha pale pale anasema, “lakini hasa ni watatu”. Yaani anaamini Mungu ni mmoja mwanzoni mwa maneno yake, kisha pale pale anakanusha imani hiyo, kwa kusema (pia) anaamini ni watatu.

Kisha anakanusha hata hayo maneno yake kwa kusema, “ Yesu ni mtoto wa Mungu.”

Kisha atakanusha hata hayo kwa kusema, “Yesu ndiye Mungu Pekee”. (Yaani maneno ya ujanja, ya Mtu kigeugeu.)

 SEHEMU YA KUMI NA TATU

Unapomuuliza kwa nini anamsifu Mungu kwa sifa ya Binadamu (sifa ya Kuzaa Mtoto), na hali Mitume wa Mungu, tangu hapo zamani, walimsifu Mungu kwa sifa zilizo bora kabisa?

Anasema, “kwa sababu Yesu alizaliwa bila ya Baba.”

Lakini tunapoangalia maumbile ya Adam, kwa mfano, tunaona kuwa ameumbwa bila ya Baba wala Mama.

Na mkewe Hawa ametolewa katika mbavu za Adam. Kwa hivyo anaye Baba, yaani Adam, lakini hana Mama.

Na Yesu kristo anaye Mama lakini hana Baba.

Kwa hivyo muujiza wa kuzaliwa Yesu bila Baba sio mkubwa kuliko wa Adam, wala wa Hawa.

Kwa hivyo ukweli ni kwamba Yesu ni mwana wa Mariam, kwa sababu maneno ya kusema Yesu mtoto wa Mungu, yanayo hatari ya binadamu kuwa anamtusi Mungu, kwa kumsifu kwa sifa ya upungufu, sifa za viumbe wake na hali ya kuwa Mungu ni mkamilifu, ahitaji Mtoto wala chochote. Kwa kuwa anajitosheleza bila mke wala chakula wala hewa.

 SEHEMU YA KUMI NA NNE

 JE! MUNGU ANA WATOTO?

Hebu tujiulize, vipi anafikia mtu kuitwa mtoto wa fulani?

Je! Wewe unaweza kumwita mtu yeyote anayepita “ Mtoto wangu?” La!

Kwa nini?

Kwa sababu mtoto kuwa ni wako, sharti kwanza utimize masharti fulani kadha wa kadha.

Kama vile; uwe umemuowa mama yake, na uyafanye naye yanayofanywa, au sivyo?

Kwa hivyo, ikiwa tunafahamu kwamba aliyeumba Mbingu na Nchi, sifa zake lazima ziwe ni zile bora (mwisho wa ubora), matusi kwa Mola yatapatikana atakapojaribu mwanadamu kusema au kumaanisha (hata kama hakusema) kwamba Mola wa ulimwengu (na Mola atuepushe mbali na maneno kama hayo) kuwa ana Mtoto, kwa sababu ikiwa hukumuowa mama yake, vipi itasemwa kuwa mtoto atakayezaliwa (wewe) ndiye baba yake?

Kwa hivyo Yesu ni mwana wa Mariam, kama inavyosema Qur’an. Na kwamba yeye ni Mtume wa Mungu, aliyezaliwa kwa miujiza ya Mungu bila baba, yaani kama Adam na hawa.

 SEHEMU YA KUMI NA TANO

Hebu angalia wanavyosema (viongozi wa kikristo) wanapohubiri;

Kama ulivyotangulia kuona, Muhubiri anaanza kwa kusema “Mungu ni mmoja.”

 Kisha anaendelea na kusema “lakini ni watatu,” maana yake, anaamini mwanzo wa maneno yake kuwa, Mungu yupo na kwamba ni mmoja.

Kisha pale pale anayakanusha aliyoyasema (mwanzo).

Na hapa ndio anapoanza mtindo wake wa kuwa kigeugeu kwa sababu anasema, “Lakini (kusema ukweli) ni watatu.”

Na anaendelea kuyakanusha hata hayo kwa kusema, “Lakini Yesu ni Mtoto wa Mungu.” Yaani (sasa anamini kuwapo) Mungu wawili na mmoja asiyekuwa kamili bado?

Kisha anaweza hata kuendelea na kusema Yesu ndiye Mungu!

Kama kungekuwa na Mungu zaidi ya mmoja, kila mmoja angetaka mambo yake (yaende) tofauti na (huyo anayedaiwa ni) mwenzake, na ingepatikana hata ugomvi kati yao.

Roho takatifu ni Malaika Jibril (Gabriel). Kwa sababu yeye anayo majina mawili. Jibril au Roho Takatifu.

 SEHEMU YA KUMI NA SITA

Kwa hivyo ikiwa Yesu ni Mungu, hebu tuone yale Mitume wote wa Mungu waliyowafahamisha watu wa enzi yao kuhusu alivyo Mungu wa kweli (How the Messengers of God described the Lord of the Universe.)

Kwanza maneno ya Mitume wote yanakubaliana kwamba, Mungu anao uhai wa milele, au sivyo?

Maana yake, hawezi kupatwa na mauti. Je! Mungu anaweza kufa?

Kisha muhubiri anayesema Yesu ni mungu hamalizi mahubiri yake ila atasema,“Yesu alikufa Msalabani.”

Kwa hivyo, maneno yake hayo yatakuwa yanamaanisha (hata kama hakusema) kwamba sifa yake (Yesu) hailingani na sifa ya Mungu. (yaani Yesu anaweza akapatwa na Mauti na Mungu hapati Mauti milele.)

Kwa sababu ikiwa kutakuwa na wakati Mungu alipatwa na mauti, basi sifa ya kuwa anao uhai wa milele itakuwa hakuna. Na hiyo ndiyo sifa mwanadamu huyu anayojaribu kuondoa katika akili za watu ili (watu) wawe na shaka kuhusu uhai wa Mola wao.

Sifa nyengine anayosifika nayo ni kwamba, Mungu halali.

Kwa sababu moja katika sifa zake ambazo ni nzuri sana, ni kwamba anajua kila kitu. Maana yake, yeye siyo sawa na Binadamu.

Kwa sababu ikiwa Mungu atalala, je! Atakuwa bado na sifa ya kuwa anajua kila kitu?

Je! Enyi Wahubiri, Yesu alilala?

Ikiwa mtasema kuwa alilala, basi maana ya maneno hayo ni kuwa Yesu sio Mungu, (hata kama hamkusema hivyo), kwa kuwa alikuwa analala, na hivyo hajui kila kitu, na kutokana na hayo atakuwa hana sifa ya Mungu, kwa sababu Mungu hajawahi kuonja usingizi wala kusinzia.

 SEHEMU YA KUMI NA SABA

Mungu ana sifa ya kuwa hali chakula. Je! Mungu anakula?

Hebu tuone kwa nini Mungu hali chakula na hali ya kuwa yeye ndiye aliyeumba kila aina ya chakula. Matunda mazuri mazuri, Nafaka, Nyama na Maji.

Na tunapoangalia binadamu anavyokipenda chakula, tunaona vile yeye huwa anapigana kwa sababu ya hiki chakula. Ndugu anamuuwa nduguye kwa sababu ya shamba. (Na hutokea pia) Waziri wa nchi (anashawishika hadi) anaiba Mali ya umma, ili aweze kuwa na Nyumba Ng’ambo, apate huko chakula kizuri. Na jambazi linaiba mobile ili liweze kununua chakula. Je! Mungu anakula?

 Mitume walisema La! Kwa nini? Kwa sababu Mungu anayo sifa ya Utakatifu. Na yeyote anayekula, baada ya masaa machache, lazima ataenda kwa choo - au sivyo?

 Kwa hivyo Mungu, haistahili kumsifu kwa sifa mbaya, kama hii ya kula chakula!

Wahubiri, je! Yesu alikula?

Ikiwa alikuwa anakula, sifa yake ya kula inamaanisha hata chooni alikuwa anaenda. Na hivyo sifa ya utakasifu aliyonayo Mungu, Yesu (ni Mwanadamu) hana.

Hayo pia yanathibitisha kwamba hata yule wanayemwita Baba mtakatifu, ikiwa anakula chakula, utakatifu utapatikana vipi?

 SEHEMU YA KUMI NA NANE

Maandiko yanasimulia kwamba Yesu alitahiriwa. Kwa hivyo wanaposema wahubiri kwamba Yesu alitahiriwa, watakuwa wanamaanisha nani aliyemtahirisha, na ni nani mtahiriwa?

Je! Wahubiri hawa huwa na fikra gani wanaposema Yesu alitahiriwa – kisha waseme Yesu ni Mungu?

Kama Yesu ni Mungu na iwe ndiye ametoa amri ya watu kutahiri, itakuwaje yeye atahirishwe na mwanadamu?

Je! Mungu – Mungu sio cheo anachopewa yeyote tunayemtaka akipate – kwa hivyo nani aliye na ujasiri wa kusema maneno makubwa kama hayo wanayosema wahubiri hawa?

Maandiko yasema Yesu alitahiriwa, Je! Wewe waonaje? Yesu ni Mungu?

(awatie Motoni)
(Nabii Isa)
(mtumwa)

Kwa hivyo kama tunavyoona, kwa ushahidi wa maneno ya Mungu, Mitume wote na Manabii wa Mungu ni Wanadamu waliochaguliwa kumtumikia Mola wa Ulimwengu. Na Yeye ndiye Amewaita Watumishi au Watumwa wake kama walivyo viumbe wote Watumwa Wake.

 SEHEMU YA KUMI NA TISA

Mungu ana sifa ya kuwa mwenye Nguvu zote, asiyeshindwa na chochote.

Wahubiri Wakristo wanasema Yesu alipokuwa mdogo, Mfalme alikuwa anawauwa watoto wa kiume hadi Yeye na Mama yake na Yusuf (baba wa kambo) ikawabidi kuhama kwa siri, kwenda Misr, hadi alipokufa Herode.

Kwa hivyo ikiwa wahubiri wanasema Yesu ni Mungu, maneno yao hayo yatakuwa yanamaanisha kwamba Mungu alikuwa anaenda Misri kwa kuogopa Nani? Askari wa Waroma?

Je! Mungu anatoroka kwa khofu? Je! Mungu anayo sifa ya uwoga? Kisha khofu ya kuwaogopa askari wa kiroma?

 SEHEMU YA ISHIRINI

Kwa hivyo maneno ya Mtume Muhammad, Swalla Allahu alaihi wa sallam, ndiyo ya kweli kuwa HAKUNA ALIYE NA HAKI YA KUABUDIWA ILLA ALLAH na KWAMBA HAKIKA MUHAMMAD S.A.W. NI MTUME WA ALLAH.

 NA KUWA ISSA MWANA WA MARIAM SIO MWANA WA MUNGU BALI NI MTUME WA ALLAH ( aliyetumwa kwa Wayahudi, ambao walimkataa).

Maneno haya ndiyo (Itiqadi) anayotamka Mtu ili kuingia katika Uisilamu.

Sio kama wanavyoeneza maadui wa hii Dini kwamba, mtu huvunjiliwa nazi kichwani au hufedheheshwa wakati wa kujiunga kwake katika Dini ya Allah.

Hayo ni maneno ya uzushi wanayoyasema, ili kuwavalisha watu hatamu za ki-fikra kwa lengo la kuwatia (walio dhaifu kati yao) khofu au chuki ili kuwazuilia wanaotaka kujiunga au kujisalimisha kwa amri ya Mola wao. Mola Ambaye ndiye mwenye uwezo wote, na ndiye mlinzi asiyeshindwa.

Kwa hivyo ikiwa umeyafahamu hayo yaliyo katika makala haya na ungependa kuwa Muisilamu, nasi tunakunasihi (tunakushauri) usipoteze muda wako, kwa ubishi au uzushi wala upuuzi na watu wale wanaopenda mambo kama hayo.

Na badala yake ufanye haraka kuamini kwamba Mungu yupo, na kwamba Yeye ni Mmoja. Na hakuna Mungu mwengine ila Yeye. Hana Mshirika katika Ufalme Wake, wala hafai kuabudiwa asiyekuwa Yeye.

Na kuamini kwamba Allah Anazo sifa nyingi, zote za ukamilifu na wala hana hata sifa moja ya upungufu kama wanavyomsifu kwa sifa kama hizo baadhi ya Wahubiri kwa lengo la kupotosha Watu kuhusu itiqadi zilizo sahihi ili wafaulu kuchuma mali yao bila kujali kwamba matokeo ya kutenda mambo kama haya, kwa wote wanaopotoka na kupotasha ukweli wa maneno ya Allah, ni kuingia katika Moto wa Jahannam.

Kisha uamini na Mitume wa Mungu wote bila kuwabagua, kama walivyofanya (Wayahudi) kumhusu (Yesu) Nabii Issa. Na kama walivyofanya (Wakristo) kumhusu Mtume wa Mwisho, Muhammad, (Swalla Allahu alayhi wa Sallam).

Na mwisho tunakupasha habari njema (mapema), kwamba unakaribishwa, kwa moyo mkunjufu, na sisi ndugu zako katika IMAAN.

ASSALAAMU ALAYKUM WA RAHAMATULLAHI WA BARAKAATUH.

Risala hii imekamilika

Tarehe 27/3/2007 yaani 8/3/1428 H,

kwa Uwezo wa Allah, Sub-hanahu wa Taala. Naye Ndiye anayestahiki shukrani zote.

Mwandishi: SALEH M. KYAMBO

email : risala fupi @ tala.yahoo.com

Mobile : +254727 253 993

Or +966594370352